Header Ads

Headline
recent

Simba kamili gado Afrika Kusini, Niyonzima, Okwi wakujiunga na timu

Nyota wawili wa kutumainiwa katika kikosi cha Simba ambao usajili wao klabuni hapo hivi karibuni ulikuwa gumzo,  Mnyarwanda, Haruna Niyonzima pamoja na Mganda, Emmanuel Okwi wanatarajia kujiunga na timu hiyo kesho Jumamosi huko Afrika Kusini.
   
Kikosi cha Simba kipo nchini humo kikijifua kwa ajili ya msimu ujoa wa Ligi Kuu Bara unaotarajia kuanza kutimua vumbi Agosti 26, mwaka huu lakini pia michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Habari za kuaminika kutoka ndani ya Simba, zimedai kuwa wachezaji hao watajiunga na timu hiyo baada ya kumalizika kwa masuala yao mbalimbali yalioyokuwa yakiwakabili.
“Niyonzima alikuwa akikabiliwa na suala la kimkataba kwani mkataba wake na Yanga ulikuwa uhajamalizika lakini leo Julai 28 ndiyo unafikia tamati hivyo kesho, Jumamosi atajiunga na timu huko Afirika Kusini baada ya kuwa huru.
“Tiketi yake ya safari tumemtumia tangu siku ya Jumanne, lakini pia Okwi naye atajiunga na timu hiyo kesho kutokana na kumalizika kwa zoezi la utoaji wa tuzo kwa wachezaji wa Uganda waliofanya vizuri katika ligi kuu ya nchi hiyo.
“Zoezi hilo ndilo lililomchelewesha kujiunga na timu kwa sababu alikuwa akiwania tuzo ya mchezaji bora wa ligi kuu ya nchini hiyo, hata hivyo leo hii ameondoka na tayari ameshafika Afrika Kusini,” kilisema Chanzo hicho cha habari.


No comments:

Powered by Blogger.