Header Ads

Headline
recent

CONTE KUJA NA ‘SURPRISE’ LIGI YA MABINGWA ULAYA



KOCHA Mkuu wa Chelsea, Antonio Conte, amesema kesho Jumanne atafanya ‘surprise’ pale kikosi chake kitakapokuwa mchezo wao wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Qarabag FK ya Azerbaijan.
CONTE

Conte amepanga kufanya surprise hiyo kwa kuwachezesha wachezaji tofauti na waliozoeleka ili kupata muda wa kuyapumzisha majembe yake kwa ajili ya kuyatumia wikiendi ijayo pale watakapokuwa na kibarua cha kupambana na Arsenal.
WACHEZAJI WA CHELSEA

“Itanilazimu kubadili kikosi, kucheza mechi saba ndani ya siku 21 si kitu rahisi,” alisema Conte na kuongeza.
“Kipindi cha nyuma kabla ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, nilikuwa nawapumzisha wachezaji wangu, lakini kwa England ni ngumu kuwapumzisha wachezaji muhimu. Unaweza kuchezesha timu ya kawaida na ukapoteza.

“Tumecheza mechi mbili tayari, kisha inafuata mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, kisha dhidi ya Arsenal Jumapili, halafu tunacheza Kombe la Carabou, halafu mechi zingine mbili za ligi kuu kabla ya kukutana na Atletico Madrid.”

No comments:

Powered by Blogger.