Header Ads

Headline
recent

Tambwe arejea uwanjani kuiokoa Yanga



Straika wa kimataifa wa Yanga, Mrundi, Amissi Tambwe tayari ameanza mazoezi mepesimepesi baada ya kupata nafuu ya tatizo la goti lililokuwa likimsumbua kwa muda.

Tambwe alipata tatizo hio hivi karibuni wakati alipokuwa na timu hiyo Kisiwani Pemba akijiandaa na mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Simba ambayo iliyofanyika siku chache zilizopita.

Tambwe amesema hivi sasa anaendelea vizuri baada ya kupata matibabu na tayari ameshaanza kufanya mazoezi mepesimepesi ya gym chini ya jopo la madakitari wa Yanga.

Amesema anajitahidi kuzingatia maelekezo yote anayopewa na madaktari hao ili aweze kurejea uwanjani mapema kwa ajili ya kuiongoza timu hiyo kuibuka na ushindi katika mechi zake zote za ligi kuu lakini pia kuishusha Simba kutoka katika nafasi ya kwanza ambayo inaishilia hivi sasa.


No comments:

Powered by Blogger.