Header Ads

Headline
recent

Begi lamzuia Mghana wa Simba kufanya mazoezi





WAKATI Kocha Mkuu wa Simba, Mcameroon, Joseph Omog akijipanga kumtumia mshambuliaji wake mpya raia wa Ghana, Nicholaus Gyan dhidi ya Azam FC, mchezaji huyo juzi Jumamosi alishindwa kufanya mazoezi na timu hiyo kwa sababu ya begi.
Gyan ambaye amesajiliwa na Simba hivi karibuni akitokea Ghana hakuweza kufanya mazoezi na timu hiyo baada ya kukosa vifaa vya mazoezi kutokana na kupotelewa na begi lake liliokuwa na vifaa hivyo pamoja na nguo zake za nyumbani wakati alipokuwa safarini akitokea kwao nchini Ghana.
Kutokana na hali hiyo alijuka akiwa mtazamaji wakati wachezaji wenza wa Simba walipokuwa wakijifua kwa ajili kujiandaa na  mechi yao ya ligi kuu dhidi ya Azam ambayo awali ilikuwa imepangwa kufanyika Jumatano hii lakini sasa imesogezwa mbele mpaka Jumamosi, Septemba 9, mwaka huu.
Gyan amekumbana na balaa hilo Jumamosi alfajiri baada ya kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam (JNIA) akitokea Ghana ambapo hakuweza kuliona begi lake hilo.
Kitendo hicho kinadaiwa kumvuruga vilivyo jambo ambalo pia lilimsikitisha Omog ambaye alikuwa akimusubilia kwa hamu kubwa mchezaji huyo katika mazoezi hayo.
Omog alisema kuwa uongozi wa timu hiyo unalishugurikia suala hilo ili Gyan aweze kupata begi lake hilo lakini pia kwa upande wake yeye anajipanga kuhakikisha ana mweka sawa kiakili  ili aweze kumtumia kwenye mechi hiyo dhidi ya Azam.
“Taarifa za kupotelewa begi lake nimezisikia lakini najua uongozi utakuwa unalishugurikia ila binafsi nimefurahia ujio wake na sasa najipanga kuhakikisha anakuwa sawa kwa ajili ya mechi yetu dhidi ya Azam.
“Niniajitahidi kumweka sawa kiakili ili aweze kusau suala hilo lilomtokea kabla ya kukabiliana na Azam, kwani tunakata kupata ushindi dhidi yao ili tuendelea kuwa juu katika msimamo wa ligi,” alisema Omog
Chanzo: Championi

No comments:

Powered by Blogger.