Header Ads

Headline
recent

Tambwe, Chirwa wawatuliza Yanga



WASHAMBULIJI wa kutumainiwa wa Yanga, Obery Chirwa pamoja na Amissi Tambwe leo hii wataungana na kikosi hicho mazoezi ya kujiandaa na mechi yao Ligi Kuu Bara dhidi ya Njombe Mji katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Yanga na Njombe Mji zitapambana Jumamosi ijayo katika Uwanja wa Sabasaba mijini Njombe baada ya Shirikisho la Soka Tanzania kuifanyia mabadiliko ratiba ya ligi kuu ambapo awali ilikuwa zipambane Jumatano hii.

Kitendo hicho cha nyota hao kujiunga na kikosi hicho kimepokelewa kwa mikono miwili na viongozi wa benchi la ufundi la timu hiyo baada ya kuwakosa kwa kipindi kirefu kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya goto.

Majeraha hayo yaliwafanya wawe nje ya uwanja kwa kipindi kirefu huku wakishindwa kuitumikia timu yao hiyo katika mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Simba lakini pia ule wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Lipuli FC.

Daktari wa Yanga, Edward Bavu alisema kuwa wachezaji hao kwa pamoja leo hii waanza mazoezi baada ya kupona majeraha yao.

“Hakika tunamshukuru Mungu kwa hilo kwani, kwani wamerejea katika kipindi muafaka baada ya kupona majeraha yao gati.

“Kwa hiyo, mpaka kufikia hapa kazi iliyobakia ni kwa makocha kuhakikisha wanawapatia mazoezi ya ufiti kabla ya kuanza kuwatumia katika mechi zijazo,” alisema Bavu na kuongeza kuwa.

“Wachezaji ambao tutaendelea kuwakosa ni kikosini kwetu ni kipa Beno Kakolanya na Geofrey Mwashiuya ambao wote bado ni majeruhi na wanaendelea na matibabu,” alisema Bavu.

Chanzo: Championi

No comments:

Powered by Blogger.