Header Ads

Headline
recent

Yanga yaipiga mkwara Bodi ya Ligi



Uongozi wa klabu ya Yanga umeitaka Bodi ya Ligi Tanzania (TPBL), pamoja na Kampuni ya Vodacom Tanzania kuiandikia barua klabu hiyo ya kuiomba radhi klabu hiyo kwa kitendo kilichojitokeza juzi Alhamisi katika hafla ya kukabidhi vifaa vya michezo kwa timu zinazoshiriki Ligi Kuu Bara.

Katika hafla hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Yanga haikuwakilishwa na kiongozi wake yeyote kutokana na kilie kilichodaiwa kuwa haikupewa taarifa za kuwepo kwa tukio hilo na badala yake Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba ambayo ni mahasimu wao kubwa, Haji Mara aliamua kujitolea kuwawakilisha watani zao hao wa jadi.

Kitendo hicho cha Manara kuiwakilisha Yanga katika hafla hiyo kimewakera vilivyo viongozi wa Yanga na kuona kama vile klabu yao hiyo imedhalilishwa na kushushwa hadhi yake iliyonayo katika soka la Tanzania ukilinganisha na timu nyingine zote zinazoshiriki ligi kuu ikiwemo Simba.

Akizungumza na Waandishi wa Habari  leo, Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Mkwasa alisema kuwa kutokana na hali hiyo, uongozi wa Bodi ya Ligi pamoja na Vodacom  wanatakiwa kuiomba klabu hiyo.

Alisema endapo watashindwa kufanya hivyo basi, watalazimika kuchukua hatua kali ikiwa ni pamoja na kwenda mahakamani kuishitaki Bodi ya Ligi pamoja na Vodacom kwa kitendo chao cha kumuruhusu Manara kuwakirisha Yanga katika zoezi hilo pasipo kuwasiliana na uongozi wa klabu hiyo.

“Jambo hilo kusema kweli lilitusikitisha sana kwani limetudhalilisha sana na limevunja hadhi ya klabu ya klabu yetu ambayo tumeitafuta kwa muda mrefu ukilinganisha na timu nyingine zinazoshiriki ligi kuu.

“Tunawaomba wa Bodi ya Ligi na Vodacom kutuandikia barua ya kutuomba radhi kwa hilo lakini pia kutusafisha kwa kashifa waliyoieneza kuwa tulishindwa kutokea katika hafla hiyo wakati hatukupewa taarifa yoyote ile juu ya kufanyika kwa hafla hiyo, kama watashindwa kufanya hivyo nadi tutachukua hatua zaidi ikiwa ni pamoja na kwenda mahakamani kutokana na udhalilishwaji huo,” alisema Mkwasa.

Katika hatua nyingine Mjumbe wa Kakati ya Utendaji wa Yanga, Salum Mkemi aliongeza kuwa hivi sasa wapo katika mchakato wa kuwasiliana na wanasheria mbalimbali wa klabu hiyo ili kuona ni hatua zipi zinastahili kuchukuliwa kwa Bodi ya Ligi na Vodacom kama watashindwa kuomba radhi

No comments:

Powered by Blogger.