Header Ads

Headline
recent

Vodacom Yagawa Vifaa Kwa Timu za Ligi Kuu


 Kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi ya Vodacom leo imegawa vifaa kwa
timu 16 zitakazoshiriki ligi kuu msimu huu wa 2017/2018.
Vifaa hivyo ni jezi, sare za mazoezi, viatu, mabegi, trakisuti, soksi, vilinda ugoko na
sare za waamuzi.
Mkurugenzi wa idara ya masoko wa Vodacom, Hisham Hendi alisema kuwa kampuni
yake imejipanga kuhakikisha mchezo wa soka unapiga hatua nchini.
"Kuelekea msimu ujao Vodacom imejipanga kufanya mambo makubwa zaidi kwenye
ligi tukiamini mchezo wa soka unaunganisha watu lakini pia ni ajira.
Tumewaandalia mambo mazuri mashabiki wa soka ambao wengi ni wateja wetu,"
alisema Hendi.
Mkurugenzi mtendaji wa bodi ya Ligi Kuu, Boniface Wambura alisema kuwa
watahakikisha wanatatua changamoto zilizojitokeza msimu uliopita.
"Changamoto kubwa ilikuwa ni waamuzi, lakini tayari tumeshakutana na kamati ya
waamuzi ili kuhakikisha tunapata waamuzi watakaokidhi viwango," alisema
Wambura.
Ofisa habari wa Simba, Haji Manara akizungumza kwa niaba ya klabu, alitoa wito
kwa bodi ya ligi kutobadilisha ratiba.
Hii inaziumiza timu ambazo hazina uwezo wa kifedha na kufanya ligi kupoteza
ushindani. "alisema Manara".

No comments:

Powered by Blogger.