Header Ads

Headline
recent

MVUA YA MABAO 'YANYESHA' USIKU WA ULAYA LEO



LIGI ya Mabingwa Ulaya, imeendelea usiku wa Oktoba 17, mwaka huu ikiwa ni hatua ya makundi ambapo zilipigwa mechi nane za Kundi E, F, G na H huku ikishuhudiwa mvua ya mabao kwa baadhi ya meci hizo.
Maribor vs Liverpool

Katika Kundi E, Liverpool ikiwa ugenini, iliibuka na ushindi mnono wa mabao 7-0 dhidi ya Maribor, huku Spartak Moscow ikiichapa nyumbani Sevila kwa mabao 5-1.
Man City vs Napoli

Feyenoord iliyopo Kundi F, imekubali kichapo cha mabao 2 – 1 kutoka kwa Shakhtar Donetsk, huku Manchester City ikiichapa Napoli mabao 2 – 1.
RB Leipzig vs Porto

Monaco ikiwa nyumbani, imechapwa 2-1 na Besiktas, wakati RB Leipzig ikiinyuka Porto mabao 3 – 2. Hilo ni Kundi G. 
Madrid vs Tottenham

Kwenye Kundi H, mechi zote ziliisha kwa sare ambapo matokeo yake yalikuwa hivi; APOEL Nicosia 1 – 1 Borussia Dortmund na Real Madrid 1 – 1 Tottenham Hotspur.

No comments:

Powered by Blogger.