Header Ads

Headline
recent

Zullu apigwa chini rasmi Yanga

Wakati dirisha la usajili kwa timu za Ligi Kuu Bara likitarajiwa kufungwa kesho Jumapili, Agosti 6, uongozi wa Yanga jana umetangaza rasmi kuachana na kiungo wake wa kimataifa raia wa Zambia,  Justine Zullu.



Yanga imefikia hatua hiyo baada ya kutolizishwa na kiwango cha mchezaji huyo aliyejiunga na timu hiyo msimu uliopita katika dirisha dogo la usajili akitokea Zesco FC ya Zambaia kwa ajili ya kuimarisha safu yake ya kiungo mkabaji ambayo imekuwa ikiitesa kwa muda mrefu.

Hata hivyo, mara baada ya kujiunga na timu hiyo Zullu, alishindwa kuonyesha ubora wake uwanjani kama Yanga walivyotarajia kuuona kutoka kwake.

Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Mkwasa amesema kuwa kutokana na hali hiyo wameamua kuachana na mchezaji huyo na nafasi yake itachukuliwa mchezaji mwingine ambaye muda wowote kuanzia leo watamtangaza kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili hiyo kesho.

“Ni kweli kabisa tumeamua kuachana na Zullu kutokana kutolizishwa na kiwango chake uwanjani kwani hakikuwa kama tulivyotajia.

“Kwa kuwa mtazamo wa klabu yetu ni kuona tunafika mbali imetubidi tufikia hatua hiyo na hivi karibuni tulizungumza na wakala wake na tumefikia makubaliano kwa hiyo hivi sasa tunachofanya ni kumalizana naye bila ya kufikishana Fifa (Shirikisho la Soka la Kimataifa),” alisema Mkwasa.

No comments:

Powered by Blogger.