Header Ads

Headline
recent

Erasto Nyoni aibeba Simba Sauzi akitoka sare na Bidvest



TIMU ya Simba imecheza mechi yake ya pili ya kirafiki dhidi ya Bidvest ya Afrika Kusini na kufanikiwa kutoka  sare ya bao 1-1.

Mechi hiyo iliyokuwa na ushindani mkubwa imeinyuka leo hii asubuhi katika Uwanja wa Sturrock Park jijini Johannesburg.

Katika mechi hiyo, Simba ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao katika dakika 33 kupitia mchezaji wake mpya, Erasto Nyoni.

Hata hivyo Bidvest walisawazisha bao hilo katika kipindi cha pili cha mchezo huo dakika ya 70.

Mechi hiyo ilikuwa ni ya pili kwa Simba tangu ilitua kwa ajili ya kambi yake ya kujiandaa na ligi kuu msimu ujoa, ambapo mechi ya kwanza ilifungwa bao 1-0 na Orlando Pirates.

No comments:

Powered by Blogger.