Header Ads

Headline
recent

KIVUMBI CHA PREMIER JANA, MAN U YAPOTEZA MECHI YA KWANZA


TIMU ya Manchester United, jana Jumamosi ilipoteza mchezo wake wa kwanza msimu huu katika Ligi Kuu England ‘Premier’ baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Huddersfield Town.


Man U iliingia uwanjani ikiwa haijapoteza mchezo hata mmoja msimu huu baada ya kucheza mechi nane na kushinda sita, huku ikitoka sare mbili na kujikusanyia pointi 20.

Vijana wa Huddersfield wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani wa John Smith, walijipatia mabao yao kupitia kwa Aaron Mooy dakika ya 28 na Laurent Depoitre (33). Bao la Man U lilifungwa na Marcus Rashford dakika ya 78.

Matokeo mengine jana yalikuwa hivi:
 
Chelsea                          4 – 2       Watford
Pedro Rodriguez 12'                                             Abdoulaye Doucoure 45'
Michy Batshuayi 71'                                              Roberto Pereyra 49'
Cesar Azpilicueta 87'
Michy Batshuayi 90'


Manchester City           3 – 0       Burnley
Sergio Aguero 30'
Nicolas Otamendi 73'
Leroy Sane 75'

Newcastle United        1 – 0       Crystal Palace
Mikel Merino 86'


Stoke City                      1 – 2       Bournemouth
Mame Biram Diouf 63'                                   Andrew Surman 16'
       Junior Stanislas 18'

Swansea City                1 – 2       Leicester City
Alfie Mawson 56'                                           Federico Fernandez 25' (OG)
      Shinji Okazaki 49'



Southampton               1 – 0       West Bromwich Albion
Sofiane Boufal 85'



Leo ligi hiyo itaendelea kwa mechi mbili ambazo ni Tottenham vs Liverpool na Everton vs Arsenal.

No comments:

Powered by Blogger.