Header Ads

Headline
recent

Omog atua Yanga kumfuata Ajibu



Bada ya hivi karibuni, mshambuliaji mpya wa Yanga, Ibrahimu Ajibu kushindwa kuiongeza timu hiyo kuibuka na ushindi dhidi ya Lipuli FC, kocha wake wa zamani Mcameroon, Joseph Omog inadaiwa kuwa anajipanga ili aweze kutua Yanga kwa ajili kufanya naye mazungumzo mafupi.

Omog ambaye ni Kocha Mkuu wa Simba na aliyekuwa akimufundisha Ajibu msimu uliopita kabla ya kujiunga na Yanga inadaiwa kuwa anataka kukutana na Ajibu ili aweze kuzungumza naye juu ya nini anachopaswa kufanya kama anataka kufanya vizuri msimu huu.

Inadaiwa kuwa Omog amefikia uamuzi huo kwa kuwa ni shabiki mkubwa Ajibu kutokana na kipaji chake na amekuwa hapendi kuona kikipotea.

Habari za kuaminika kutoka ndani ya Simba ambazo zimedai kuwa jambo kubwa ambalo Omog anatarajia kumwambia Ajibu mara tu atakapoonana naye ni kuhusiana na kubadili mfumo wake wa maisha.

“Amejaribu kumtafuta mara kadhaa kwa njia ya Simu lakini hajampata ila jambo kubwa analotaka kumwambia endapo atafanikiwa kuonana naye siku yoyote ni  juu ya kubadili mfumo wake wa maisha kama kweli anataka kufanikiwa.

“Mara nyingi alikuwa hafurahishwi na jinsi Ajibu alivyokuwa anaishi wakati alipokuwa Simba licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa kucheza soka, kwa hiyo hivi sasa anataka kumuona akiachana na maisha hayo na akili yake aweze kuilekeza zaidi mazoezini na kuzingatia yale yote anayoambiwa viongozi wake wa ufundi,” kilisema chanzo hicho cha habari.

Hata hivyo alipolizwa Omog kuhusiana na hilo alisema kuwa: “Siyo kwamba nataka kufuata Yanga ila nikipata bahati ya kukutana naye nitamshauri kuhusiana na hayo.

“Ajibu ni mmoja kati ya wachezaji wachache hapa nchini wenye vipaji vya juu hivyo siyo jambo zuri kumuacha akapotea, binafsi ni shabiki wake mkubwa na siku zote nimekuwa nikitaka kumuona afike mbali na ikiwezekana awe kama Mbwana Samatta.

“Ana kipaji cha hali ya juu hivyo ni kitendo cha yeye sasa kubadilika na kutamani zaidi mafanikio,” alisema Omog.

No comments:

Powered by Blogger.