Header Ads

Headline
recent

Mourinho azua balaa Ulaya



Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho ameonyesha umahiri wake wa kuwa kipa baada ya kushiriki mechi ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kuwasaidia watu walioathiriwa na moto wa jengo la Grenfell.

Mourinho alicheza kama kipa katika mechi hiyo Game4Grenfell kati ya timu mbili za watu mashuhuri na wacheza soka wa zamani.

Fedha zilizopatika kutokana na tikiti za mechi hiyo zilienda katika mfuko wa wale walioathiriwa na janga la moto. 

Hata hivyo katika mechi hiyo, timu ambayo alikuwa akiichezea ilishindwa kwa mabao 5-3 kwa njia ya penalty na bingwa wa olimpiki Mo Farah alifunga moja kati ya mabao hayo.

Katika ajari hiyo ya moto watu 80 walifariki.

No comments:

Powered by Blogger.