Header Ads

Headline
recent

Lwandamina arejea Yanga, aongoza mazoezi ya kuitungua Njombe Mji



KOCHA Mkuu wa Yanga, Mzambia, George Lwandamina tayari amerejea nchini akitokea kwao Zambia alipokuwa ameenda kwa ajili ya kumzika baba yake mzazi aliyefariki dunia hivi karibuni.

Katika mazoezinya ya leo ya timu hiyo yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar Lwandamina ndiye aliyekuwa akiongoza mazoezi hayo akisaidina na wasaidizi wake wa benchi la ufundi tayari kwa kuwaweka fiti wachezaji wake kwa ajili ya mechi ijayo ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Njombe Mji.

Yanga na Njombe Mji zitapambana na Jumamosi ijayo katika Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe.

No comments:

Powered by Blogger.