Header Ads

Headline
recent

Kipa kiboko ya Simba afariki dunia



SHIRIKISHO la Soka la Rwanda, (Ferwara), limethibitisha kuwa, mlinda mlango wa zamani wa Sofapaka na timu ya taifa ya Rwanda, Evariste Mutuyimana, amefariki dunia leo Jumanne akiwa nyumbani kwake, Kigali, Rwanda.

 
Mlinda mlango huyo amefariki akiwa na miaka 26 ambapo alikuwa akiitumikia Klabu ya Rayon Sports ya Rwanda kabla ya kufikwa na mauti hayo huku chanzo cha kifo chake kikitajwa kuwa ni tatizo la kushindwa kupumua vizuri kutokana na matatizo ya moyo yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda mrefu.

“Mutuyimana alikuwa na matatizo ya moyo kwa muda mrefu sasa. Kwa bahati mbaya tumempoteza. Alikuwa mlinzi mzuri na Rwanda kwa kweli imempoteza mtu muhimu,” alisema Ofisa Habari wa Ferwara, Bonnie Mugabe.

Juni, mwaka jana, Mutuyimana alijiunga na Rayon Sports inayoshiriki Ligi Kuu ya Rwanda maarufu kama Azam Rwanda Premier League baada ya kukaa kwa kipindi cha miezi 18 katika kikosi cha Sofapaka inayoshiriki Ligi Kuu ya Kenya maarufu kama SportPesa Premier League (SPL).

Mlinda mlango huyo, atakumbwa na Watanzania kutokana na miezi michache iliyopita timu yake ilipocheza dhidi ya Simba katika mchezo wa Tamasha la Simba Day na kufungwa bao 1-0, yeye alikaa langoni dakika zote tisini. Mechi hiyo ilipigwa Agosti 8, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.

No comments:

Powered by Blogger.