Header Ads

Headline
recent

Sauzi wakubali mechi yao na Senegal kurudiwa



Viongozi wa ngazi ya juu katika Shirikisho la Soka Afrika Kusini (Safa) wamekubali mechi yao ya kuwania kufuzu kushiriki Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018 ambapo Afrika Kusini iliibuka mshindi dhidi ya Senegal inastahili kurudiwa. 

Shirikisho la soka la Kimataifa FIFA limetoa ilani kwamba mechi hiyo irudiwe baada ya mwamuzi aliyechezesha mechi hiyo, Joseph Lamptey kupigwa marufuku kwa kutoisimamia vyema mechi hiyo.

Safa imekuwa ikitathmini jinsi ya kukata rufaa lakini kwa sasa imesema imekubaliana na Fifa.

Hata hivyo shirikisho hilo limesema lingekata rufaa iwapo mashtaka ya mwamuzi huyo yangebatilishwa.
Afrika Kusini iliichapa Senegal magoli 2-1 katika mechi waliotoka sare mwaka jana.

No comments:

Powered by Blogger.