Header Ads

Headline
recent

Lwandamina azushiwa kutimuliwa Yanga




SIKU moja baada ya mchezo wa Ngao ya Jamii, kuliibuka taarifa kuwa Kocha wa Yanga, George Lwandamina alikatiwa tiketi ya ndege ya kuondoka Dar kwenda kwao Zambia.

Hata hivyo Lwandamina amekanusha madai hayo na kudai kuwa hayana ukweli wowote.

Taarifa za awali zilianza kusambaa baada ya kuonekana nakala ya tiketi ya Kampuni ya Fastjet ikionyesha kocha huyo anatarajia kuondoka leo Ijumaa saa 4:50 usiku kuelekea Zambia ambapo angefika kesho Jumamosi saa 6:20 usiku.

Tiketi hiyo ambayo inaonyesha namba ya ndege ambayo ni FN0250, inaonyesha jina la kocha huyo ambaye ndiyo msafiri na malipo yake yalitakiwa kufanywa jana Alhamisi kabla ya safari hiyo.


Uongozi wa Yanga ulikanusha taarifa hizo na alipotafutwa Lwandamina mwenyewe alisema: “Watu wengine huongea kwa niaba yangu.” Alipotumiwa nakala ya tiketi akajibu: “Hiyo ni tiketi bandia.” 


No comments:

Powered by Blogger.