Header Ads

Headline
recent

Hawa Ndiyo Viongozi Wapya wa Shirikisho la Soka Tanzania(TFF)


 
Rais wa TFF, Wallace Karia
Makamu wa Rais TFF, Michael Richard Wambura

Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini, wakili Revocatus Kuuli ametangaza matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa chama hicho uliofanyika leo katika Ukumbi wa Hosteli za Chuo cha Mtakatifu Gasper mjini Dodoma.
Revocatus Kuuli wakati akitangaza matokeo ya nafasi ya urais wa TFF amesema kwamba jumla ya kura zilizopigwa ni 128 ambapo kura halali ni 125 na kura zilizoharibika ni 3.
Katika kura hizo 125, Wakili kuuli alimtangaza Rais mpya wa Shirikisho hilo kuwa ni Wallace Karia ambaye ameshinda nafasi hiyo kwa jumla ya kura 95 kati ya kura halali 125 zilizopigwa. Wagombea wengine wa Urais pamoja na kura walizopata kwenye mabano ni Ally Mayay Tembele (9), Shija Richard (9), Iman Madega (8), Frederick Mwakalebela (3) na Emmanuel Kimbe (1). Ndugu Michael Wambura amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Shirikisho hilo.
Wajumbe wa Kamati ya Utendaji walioshinda kwenye uchaguzi wa leo pamoja na Kanda wanazoziwakilisha kwenye mabano ni kama ifuatavyo:
Mohamed Abeid (Dodoma na Singida), Mbasha Matutu (Shinyanga na Simiyu), Sarah Chao (Arusha na Manyara), Dustan Ditopile (Lindi na Mtwara), Elias Mwanjala (Mbeya na Iringa), Francis (Pwani na Morogoro), Vedastus Lufano (Mara na Mwanza), Lameck Nyangaya (Dar es salaam), Kenneth Pesambili (Rukwa na Katavi), Khalid Mohamed (Kilimanjaro na Tanga), Issa Mrisho (Kigoma na Tabora) na James Patrick (Njombe
Rais wa Shirikisho hilo, Wallace Karia, Makamu wa Rais, Michael Richard Wambura pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji waliochaguliwa wameapishwa leo mjini Dodoma muda mfupi baada ya matokeo ya ushindi wao katika uchaguzi huo kutangazwa.
Akitoa hotuba yake muda mfupi baada ya kuapishwa kwake, Rais wa Shirikisho hilo (Wallace Karia) amesema kuwa amepigiwa simu na Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Gianni Infantino pamoja na Rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Ahmad Ahmad na wote wamelipongeza Shirikisho hilo kwa uamuzi ulioufanya na kuutakia uongozi mpya mafanikio mema.

No comments:

Powered by Blogger.