Header Ads

Headline
recent

UTAMU WA FDL WIKIENDI HII HUU HAPA


RAUNDI ya Sita ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL), itaendelea wikiendi hii kwa kupigwa mechi kadhaa kwenye viwanja tofauti.

Katika Kundi A, Mvuvumwa FC ya Kigoma, watacheza na Mgambo JKT katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Mechi nyingine kwenye kundi hilo itafanyika kesho Jumapili Oktoba 22, mwaka huu kwa michezo mitatu.

Mechi hizo ni kati ya Kiluvya United na Mshikamano  kwenye Uwanja wa Filbert Bayi, Pwani. African Lyon  itacheza na Ashanti United  kwenye Uwanja wa Uhuru, wakati Friends Rangers itapambana na JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Azam, Dar es Salaam.

Katika Kundi B, leo Jumamosi, Mbeya Kwanza itacheza na JKT Mlale katika Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi, Pwani na Jumapili Polisi Tanzania watawakaribisha KMC kwenye Uwanja wa Ushirika, Moshi, huku Mawenzi Market wakiwaalika Mufindi United kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

Katika Kundi C, michezo ya leo Jumamosi  itazikutanisha Biashara Mara dhidi ya JKT Oljoro kwenye Uwanja wa Karume, Mara, Transit Camp itakuwa mwenyeji wa Dodoma FC kwenye Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, huku Toto Africans ya Mwanza itacheza  na Rhino Rangers ya Tabora katika mchezo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.

No comments:

Powered by Blogger.