Header Ads

Headline
recent

KOCHA KOEMAN ATIMULIWA EVERTON



KLABU ya Everton imetangaza kumfuta kazi kocha wa timu hiyo, Ronald Koeman.

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni saa chache baada ya timu hiyo kukubali kichapo cha mabao 5-2 kutoka kwa Arsenal kwenye mchezo wa Ligi Kuu England ‘Premier’ uliopigwa jana Jumapili katika Uwanja wa Goodison Park.
 
...akiwa na mkewe
Makocha wanaotajwa kwenda kuchukua nafasi yake ni Kocha wa Burnley, Sean Dyche, Eddie Howe (Bournemouth) na Marco Silva (Watford).
 
...akielekea mazoezini leo asubuhi
Leo asubuhi, kocha huyo kama kawaida alifika katika uwanja wa mazoezi wa timu hiyo kwa ajili ya mazoezi ambapo alikutana na mwenyekiti wa klabu hiyo, Bill Kenwright na Mtendaji Mkuu, Robert Elstone, wakafanya kikao.

Baada ya kikao hicho, mchana klabu hiyo ikatoa taarifa ya kufukuzwa kwa kocha huyo ambayo ilisema: “Klabu ya Everton imethibitisha kwamba Ronald Koeman ameondoka klabuni.
 
Koeman
“Mwenyekiti, Bill Kenwright, bodi ya wakurugenzi na mwekezaji mkuu, Farhad Moshiri, kwa pamoja wameridhika na huduma ya Koeman kwa kipindi cha miezi 16 aliyokaa klabuni na kuisaidia timu kumaliza msimu uliopita nafasi ya saba katika Premier.”

No comments:

Powered by Blogger.