Header Ads

Headline
recent

Kakolanya naye yupo fiti, sasa Yanga kicheko tu



BAADA ya Obrey Chirwa na Amissi Tambwe kupona majeraha yao na kurejea kikosini Yanga, kipa wa timu hiyo, Beno Kakolanya naye amepona na muda wowote anatarajiwa kuanza mazoezi na wenzake.

Kakolanya aliyekuwa akisumbuliwa na tatizo la goti la mguu wa kulia, alikaa nje ya uwanja kwa zaidi ya miezi miwili tangu alipoumia akiwa na kikosi cha Taifa Stars kilichoshiriki michuano ya Cosafa, Juni, mwaka huu nchini Afrika Kusini na kushika nafasi ya tatu.

Kwa takribani wiki mbili zilizopita, Kakolanya alikuwa akifanya mazoezi ya gym baada ya kupewa programu maalum, ambapo programu hiyo aliimaliza jana Jumatatu na leo Jumanne kwa mara ya kwanza alionekana katika Uwanja wa Uhuru, wakati wenzake wakifanya mazoezi, lakini yeye akikaa nje.

No comments:

Powered by Blogger.